|
1.Ukuhani mmoja katika
Kristu,
Kwa njia ya ubatizo wanawake na wanaume wanashiriki sawa katika
ukuhani mpya wa Kristu. Hii inajumuisha utayari wao katika madaraja
matakatifu. click!
2.Wamewezeshwa
kuadhimisha
Wakati wa Karamu ya mwisho Yesu aliwawezesha wanawake na wanaume.
Wote wanaweza kupewa daraja na kuadhimisha Ekaristi.
click!
3.Upendeleo wa
Kiutamaduni Desturi ya Kanisa ya kutowapa daraja wanawake kama makuhani ililenga
vigezo vitatu vya upendeleo dhidi ya wanawake. Hii iliathiri maamuzi ya
viongozi wa Kanisa.click!
4. Wanawake walishawahi kuwa
Mashemasi Mpaka walau karne ya tisa Kanisa liliwapa wanawake sakramenti
kamili ya daraja la ushemasi. Hii inathibitisha kuwa wanawake wanaweza
kupewa daraja la upadre click!
5. Uwezo wa wanawake kupewa
daraja umekuwapo kwenye mapokeo ya Kanisa yasiyoridhiwa.
Mfano mmojawapo ni ibada ya zamani kwa Maria kama kuhani. Hii
inaonesha kwamba kulingana na hali ya waamini kwa Maria kizuizi dhidi ya
wanawake kimeshaondolewa.click!
6. Sehemu kubwa ya Kanisa
hukubali daraja la upadre kwa wanawake.
Baada ya sala na utafiti wa ndani, makanisa mengine ya Kikristu sasa
yanawapa wanawake daraja la upadre. Ijapokuwa si kila kitu ambacho makanisa
mengine yanafanya chaweza kukubaliwa na Kanisa Katoliki,makubaliano haya ya
pamoja ya waamini wa Kikristu yadhihirisha kwamba, daraja kwa wanawake ni
kulingana na mtizamo wa Kristu. click!
7. Wanawake pia,kwa
hakika, wameitwa kuwa makuhani. Ukweli kwamba wanawake wengi wawajibikaji wa Kikatoliki huamua
wenyewe wito wa upadre ni ishara ya Roho Mtakatifu ambayo hatuwezi
kuipuuza.click!
Hitimisho: Hakuna hoja halali
dhidi ya wanawake mapadre, na hamna hoja nyingi za Kikatoliki zinazounga
mkono jambo hili. |